We Like Sharing

Monday, January 23, 2017

Breaking news - vichekesho

Breaking news - vichekesho

Breaking news

Jana katika msitu wa wanyama pori wa Mikumi uliopo mkoani Morogoro ilitangazwa kuwa kuna nyoka hatari sana ambaye hajawahi kutokea popote duniani.

Mashuhuda wanadai kuwa nyoka huyo anaongezeka urefu kwa 0.5cm kila akila chakula na huwa anakula chakula kuanzia sekunde 30 kurudi nyuma.

Mpaka sasa hakuna silaha ya kuweza kumuua nyoka huyo isipokuwa akijiuma yeye mwenyewe ndio anaweza kufa. Wanasayansi walieleza japo uchunguzi bado unaendelea, na waliongeza kuwa nyoka huyo anapatikana kwenye simu za Nokia za tochi pekee katika sehemu ya Game inayoitwa Snake Xenzia.

Ha ha haaaaa. Asante kwa umakini mkubwa katika usomaji wako kwenye chapisho hili. Hiki ni kichekesho tu, tunakutakia mchana mwema.

©2016. Nzegamedia! Designed by Chris Kabeya De Pro

No comments:

Post a Comment